KIKUNDI CHA KIMATAIFA

Kikundi cha kimataifa kinachohusika na Njia kimeundwa tangu 2018 na Kiko Argüello -mwajibikaji wa Njia–, María Ascensión Romero, na P. Mario Pezzi. Tangu mwanzo wa Njia mnamo 1964, na hadi 2016, kiliundwa na Kiko Argüello na Carmen Hernández, waanzilishi wake, na pia na P. Mario Pezzi. Baada ya Carmen kufariki mnamo Julai 19, 2016, na kama ilivyoandikwa katika Statuta za Njia, María Ascensión Romero alijiunga na kikundi hicho. Kikundi hiki kinasimamia uongozi wa Njia ya Neokatekumenato duniani kote, wakishirikiana na vikundi vya makatekista wasafiri katika kila taifa. Miongoni mwa majukumu yake yapo yale ya kuongoza utekelezaji wa Njia ya Neokatekumenato na kudhamini uhalisi wake; kutimiza wajibu wao wenyewe, kama ulivyoelekezwa katika Statuta rasmi; kuomba mashauriano ambayo yanachukuliwa kuwa yanafaa; kudumisha mahusiano ya mara kwa mara na Maaskofu wa jimbo; kudumisha mahusiano ya mara kwa mara na Idara ya Walei, Familia na Uhai kutoka Kiti kitakatifu, pamoja na majukumu mengine.