Uinjilishaji

Utume wa kuinjilisha


“Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane. Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.” (Yohana 13, 34s).

Roho Mtakatifu ameinua ndani ya Njia ya Neokatekumenato aina mbalimbali za uinjilishaji, za utume wa kitume na za kuwekwa wakfu, ambazo zimethibitishwa na kusukumwa na Mapapa mbalimbali wa Kanisa.

Karama


Parokia jumuiya ya jumuiya

Baada ya tangazo la Kerigma jumuiya zinaibuka katika parokia, ndugu wanaoishi uingizwaji huu kwa ukristo. Hatua kwa hatua zinaanza kuonekana kati yao dalili za Imani, upendo kwa adui. Muujiza huu wa kiroho utawaita walio mbali kukutana na Yesu Kristo. Na jumuiya ya kikristo itabeba Upendo wa Mungu kwa watu wote.

Parokia Jumuiya ya Jumuiya

“Ninyi Hamfanyi tu utume kwa sababu ya jinsi mlivyo, katika msukumo wa kugundua na kurejesha thamani za kikristo za kweli, zilizo halisi, zenye nguvu, ambazo vinginevyo zingeweza karibu kuyeyuka katika maisha ya kawaida. Hapana! Ninyi mnaziweka kwenye ushahidi, mnazifanya zitokeze, na mnazipatia mng’ao wa kimaadili ambao ni mfano halisi kwa sababu, hivyo, pamoja na roho hii ya kikristo, mnaishi jumuiya hii ya Neokatekumenato…

Ni furaha gani na tumaini gani mnavyotupatia na uwepo wenu na matendo yenu! Tunajua kwamba ndani ya jumuiya zenu mnafanya kazi pamoja ili kuelewa na kustawisha hazina za Ubatizo wenu na matokeo ninyi kuwa mali yake Kristo…

Kuishi na kukuza mwamko huu ni kile ambacho ninyi mnaita aina ya “baada ya Ubatizo” ambayo itaweza kufanya upya katika jumuiya za kikristo za leo matokeo ya ukomavu na ya kina ambayo yalitendeka katika Kanisa la mwanzo tangu kipindi cha maandalizi ya Ubatizo…

Ninyi mnafanya baadaye: kabla au baada, Naweza kusema, si muhimu. Swala ni kwamba ninyi mnatazamia uhalisi, utimilifu, uwiano sawia, unyofu wa maisha ya Kikristo».

Mt. Paulo wa Sita, Mei 8 1974

«Uzoefu na kanuni za Kanisa vimeingiza desturi takatifu ya kutoa ubatizo kwa watoto wachanga, zikiruhusu kwamba ibada ya ubatizo ifupishe kiliturjia yale maandalizi ambayo, katika vipindi vya kwanza, wakati jamii ilikuwa ya kipagani sana, yalifanyika kabla ya ubatizo, na yaliyoitwa katekumenato. Lakini katika mazingira ya kijamii ya leo namna hii inahitaji kuunganishwa na maelekezo, na uanzishwaji unaoendana na mtindo wa maisha unaofaa kwa mkristo, ukifuata ubatizo, yaani, na msaada wa kidini, na mafunzo ya vitendo kwa uaminifu wa kikristo, na kuingizwa kwa nguvu katika jumuiya ya waumini, ambayo ni Kanisa…

Tazameni hapa kuzaliwa upya kwa jina la “katekumenato”, ambayo hakika haitaki kubatilisha au kupunguza umuhimu wa mwenendo uliopo sasa wa kubatiza, bali inataka kuutekeleza kwa mbinu ya uinjilishaji wa hatua kwa hatua na wa kina, unaokumbusha na kufanya upya kwa namna fulani ile katekumenato ya nyakati nyingine. Aliyebatizwa anahitaji kuelewa, kufikiri upya, kuthamini, ili kuunga mkono utajiri usiopimika wa sakramenti iliyopokelewa.

Mt. Paulo wa Sita, Januari 12 1977


Makatekista-wasafiri

Moja ya karama kuu au matunda ya Njia ni ile ya makatekista-wasafiri. Kupitia wao imeenea katika mabara yote matano. Kikundi cha wawajibikaji wa kimataifa cha Njia kinaunda vikundi vya makatekista wasafiri – ambavyo kwa kawaida huundwa na mpresbiteri, wanandoa na mseja (mmoja wa kiume); au mpresbiteri, mseja mmoja wa kiume na mmoja wa kike–, ili kutumwa kwa mataifa kuanzisha na kuongoza utekelezaji wa Njia ya Neokatekumenato.

Kiko Argüello, Carmen Hernández na Pd. Mario Pezzi huko Korazini

Makatekista wasafiri wanajibu hivi kwa maombi ya majimbo ya mbali: kikundi cha kimataifa kinawaalika ndugu wa Njia kujitolea ili kupelekwa popote duniani, na wale wanaosikia wameitwa na Mungu wanajitoa kwa hiari.

Wasafiri hupokea ombi hili ndani ya kuishi pamoja, na ndani yao kikundi cha wawajibikaji wa kimataifa cha Njia, au kingine kinachoteuliwa nao, kinathibitisha utayari na kuratibu shughuli za wasafiri, kwa mwendo wa “kubana na kuchia misuli ya moyo”, kwa kufuata mfano wa Bwana, aliyewatuma mitume wake kwenye utume, kisha akawakusanya mahali pa faragha, kusikiliza mambo ya ajabu ambayo Roho Mtakatifu alifanya nao.

Katekista msafiri anaendelea kuwa sehemu ya parokia na jumuiya yake, ambapo hurudi mara kwa mara kushiriki katika Njia ya jumuiya hiyo. Zaidi ya hayo, katekista msafiri anakubali kuishi utume wake katika hali habaishi, akiwa huru kuukatiza wakati wowote, akimfahamisha Askofu wa pale alipo na kikundi cha wawajibikaji wa Njia.


Karama za kimisionari na maisha ya wakfu

Katika namna mbalimbali za uinjilishaji zinazoendeshwa na Njia, unahitajika uwepo wa wanaume na wanawake waseja wenye wito wa kimisionari ili kuunga mkono, kusindikiza na kuinjilisha katika missio ad gentes na vikundi vya makatekista wasafiri, kama vile katika seminari na ndani ya parokia. Kwa sababu hiyo, katika kuishi pamoja za kimataifa wanatumwa wanaume na wanawake ambao, wakiishi njia hii ya imani, wanasikia wito wa Mungu wa kutoa maisha yao kwa Uinjilishaji Mpya.

Kwa kuongezea, tangu mwanzo wa Njia ya Neokatekumenato, mamia ya wasichana waliokuwa wakianza uingizwaji huu wa kikristo wamesikia wito kwa maisha ya kuwekwa wakfu na wameingia katika monasteri mbalimbali duniani kote.


Seminari za kijimbo za kimisionari za Redemptoris Mater

Tarehe 26 Agosti 1986, Yohane Paulo II alikaribisha kwa shauku pendekezo la Kiko, Carmen na Padre Mario la kuanzisha huko Roma Seminari ya Kijimbo ya Kimisionari kwa ajili ya malezi ya wapresbiteri kwa ajili ya Uinjilishaji Mpya na akamteua Kardinali Ugo Poletti, Askofu Msaidizi wa Baba Mtakatifu, aisimike.

Tangu hapo seminari 122 zimesimikwa, ambazo zina sifa 3 za msingi: ni za kijimbo, za kimisionari na za kimataifa. Ndani ya malezi ya kitaaluma, ya kibinadamu na ya kiroho ya seminari hizi kipo kipindi cha uinjilishaji wa kimisionari, na wakiisha pata daraja la upadre -baada ya miaka michache ya kufanya kazi katika parokia-, askofu wa jimbo anawaruhusu kuondoka kwenda kuhudumu katika namna mbalimbali za utume zinazotekelezwa na Njia ya Neokatekumenato, kulingana na yale ambayo yameidhinishwa na kupitishwa na Vatikano katika Statuta.

Seminari inasimikwa na askofu wa jimbo na inawakaribisha vijana ambao wamegundua wito kupitia safari ya neokatekumenato ya uingizwaji wa Kikristo. Katika seminari, malezi ya kikristo kupitia Njia ya Neokatekumenato ndani ya jumuiya ni kipengele maalum na cha msingi cha safari ya malezi.

Katika miaka iliyofuata, maaskofu wengi wamefuata mfano wa Baba Mtakatifu kwa kufungua seminari nyingine.

Tangu 1990, mwaka wa ibada za kwanza za kutoa daraja takatifu, hadi leo, wapresbiteri waliopata daraja katika Seminari za Redemptoris Mater ni takriban 2,380. Hivi sasa, kuna vijana 2,300 wanaojiandaa kupokea daraja takatifu.


Familia katika utume

Mwaka 1985 Kiko, Carmen na Padre Mario walimwonyesha Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili mradi – uliopokelewa kwa shauku kubwa kwa upande wake – ili kuinjilisha tena Ulaya ya kaskazini kwa kutuma familia za kimisionari zinazosindikizwa na mpresbiteri. Mnamo 1986, Papa alituma familia 3 za kwanza: moja kaskazini mwa Finland, nyingine Hamburg (Ujerumani) na ya tatu Strasbourg (Ufaransa). Mnamo 1987 familia 3 za kwanza zilitumwa kwa vile vinavyoitwa “vijiji vijana ” vya Amerika ya Kusini.

Mnamo Desemba 30, 1988, Yohane Paulo II aliwasili kwa helikopta katika Senta ya Kimataifa ya Njia ya Neokatekumento huko Porto San Giorgio kutuma familia 72 popote duniani. “Kanisa Takatifu la Mungu, wewe huwezi kufanya utume wako, huwezi kutimiza utume wako duniani, ikiwa si kwa njia ya familia na utume wake.” “Familia Takatifu si kitu kingine isipokuwa hiki: familia ya kibinadamu katika utume wa kimungu. Familia katika utume, Utatu Mtakatifu katika utume. Mnapaswa kusaidia familia, mnapaswa kuilinda dhidi ya uharibifu wowote,” alisema siku hiyo Mtakatifu Yohane Paulo II.

Tangu wakati huo, karibu familia 1,800 zimetumwa na Mapapa wa mwisho kwa mabara yote matano kuinjilisha kwa ushuhuda wao wa maisha ya kikristo kwa sura ya Familia Takatifu ya Nazareti na kupitia kazi mbalimbali za kimisionari.

Ni familia ambazo, baada ya miaka mingi katika safari hii ya malezi baada ya ubatizo, ambapo nyingi zimejengwa upya, wanashukuru kwa kazi ya wokovu ambayo Mungu amefanya ndani yao. Familia hizi, wengi wao wakiwa na watoto kadhaa, wanajitolea kwenda kwenye utume wakiacha raha ya maeneo yao ya asili. Wanaenda kwenye utume popote ambapo maaskofu wanaona haja ya ushuhuda wa familia ya kikristo, wakiishi na kukita mizizi katika makanisa mahalia na kutekeleza kazi mbalimbali za uinjilishaji, wakishiriki katika upandikizaji wa jumuiya mpya za kikristo.

Katika Statuta za Njia, imeelekezwa kwamba utekelezaji wa Njia ya Neokatekumenato unaweza kusaidiwa na familia zilizo katika utume ambazo, kwa ombi la Maaskofu, zinaenda kuishi katika maeneo yaliyoacha ukristo wao au ambapo “implantatio ecclesiae” (“kanisa kupandikizwa”) inahitajika (Kifungu cha 33 [Familia katika utume], Statuta za Njia ya Neokatekumenato, Mei 11, 2008)


Missio ad gentes (“Utume kwa mataifa”)

Mnamo mwaka wa 2006, Benedikto XVI alizindua aina hii mpya ya uinjilishaji kwa kutuma missio ad gentes 7 za kwanza. Kila moja imeundwa na mpresbiteri, akisindikizwa na familia 4 ama 5 zilizo na watoto kadhaa. Kwa ombi la askofu, familia inapokea wajibu wa kuinjilisha katika maeneo yaliyopoteza ukristo au ya kipagani, pamoja na utume wa kuonyesha jumuiya ya kikristo ambamo “wawe kitu kimoja ili ulimwengu upate kusadiki.”

Yohane Paulo II, kwenye Kongamano la VI la Maaskofu wa Ulaya la 1985, alielekeza kwamba ili kukabiliana na uduniaisho wa Ulaya ilikuwa ni lazima kurejea mfano wa kitume wa kwanza.

Utume Nyanjani Uinjilishaji

Hivyo, missio ad gentes hizi, kwa kuiga domus ecclesiae (“nyumba-kanisa”), wanakutana majumbani kati ya wasiobatizwa na waliotengwa.

Miaka kumi na miwili baada ya kutuma kwa mara ya kwanza matokeo yake ni kwamba wengi waliotengwa na wapagani ambao hawakuwahi kuingia kanisani wanajikaribisha kwenye jumuiya hizi za kikristo na kuanza safari ya wongofu ama ya kurudi kwenye imani.

Jumuiya hizi – ambazo hazijatokea kutoka eneo wakfu, bali zinaishi katikati ya ulimwengu- zinageuka kuwa”uwanda wa Mataifa ambapo watu wanaweza kumkaribia Mungu bila kumjua”, kama Benedikto XVI alivyoeleza katika hotuba yake kwa Watendaji wa Roma mnamo 2009.

Kipengele cha ajabu cha maang’amuzi haya ni matunda ya ushirika na umoja yanayotokea ndani ya familia yenyewe, kati ya wazazi na watoto.

Mnamo tarehe 18 Machi 2016, Papa Fransisko alituma familia 250 akiunda missio ad gentes 50 mpya kwa mabara matano. Wakati wa mkutano huu, Fransisko mwenyewe alieleza mtindo huu wa kimisionari unamaanisha nini: “missio ad gentes zinaundwa kwa ombi la maaskofu wa majimbo wanapokusudiwa na zinaundwa na familia 4 hadi 5 – wengi wao wakiwa na zaidi ya watoto wanne–, mpresbiteri, kijana na dada wawili. Wote wanaunda jumuiya ambayo ina utume wa kutoa ishara za imani zinazowavutia watu kwa uzuri wa Injili”, alieleza.

Papa Benedikto XVI, kutoka 2006 hadi 2012, alituma missio ad gentes 58 na Papa Fransisko ametuma 128.

Mei 5, 2018 kwenye mkutano wa kimataifa wakati wa kuadhimisha miaka 50 ya kuzaliwa kwa jumuiya ya kwanza ya Njia huko Roma, iliyoadhimishwa huko Tor Vergata (Roma), Papa Fransisko alituma missio ad gentes 34 mpya.

Idadi ya familia kwenye Njia zilizo katika utume kwa uinjilishaji mpya ni 1,668, zenye watoto takriban 6,000, katika nchi 108 kwenye mabara 5, tukihesabu pia missio ad gentes 216 katika mataifa 62.


Jumuiya katika utume

Katika mkutano na Benedikto XVI katika Basilika la Mtakatifu Petro mnamo Januari 10 2009, kwa kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 ya kuzaliwa jumuiya ya kwanza ya neokatekumenato huko Roma, zilitumwa na Baba Mtakatifu Jumuiya 15 za kwanza kwa maeneo yaliyo nje kidogo ya mji wa Roma.

Jumuiya hizi zilikuwa tayari kuacha parokia yao – ambapo tayari walikuwa wamekamilisha safari ya neokatekumenato – ili kwenda kwenye utume kwa maeneo magumu ya nje ya mji kupitia mwaliko wa maparoko. Maeneo yaliyoharibiwa, yenye ukatili mwingi, madawa ya kulevya, familia zilizovunjika, wahamiaji waliowasili hivi karibuni…

Kutumwa kwa Missio ad Gentes kutoka Basilika la Mt. Petro

Kiko, akitambulisha utume huu mpya, alisema kwamba “Njia inaisha kwa kutangaza Injili ulimwenguni kote. “Moja ya mambo mapya zaidi ni kwamba jumuiya nzima inaenda kwenye utume. Siyo baadhi ya ndugu, jumuiya nzima inaenda. Ni neema kubwa sana na ni kitu cha ajabu kwamba Mungu awatume kwa utume huu. Ni ajabu kuweza kuondoka, kwamba Bwana akupatie utume; kufa katika utume, kuzeeka katika utume.”

Kwa namna sawia, Papa Fransisko katika barua yake ya Evangelii Gaudium anazungumza juu ya Kanisa “linalotoka nje” na kuelezea hitaji la kuinjilisha maeneo ya “nje”, kijiografia na kimaisha: “

Pia jimbo la Madrid, ambapo Njia ilizaliwa na ipo katika parokia 45 zenye jumuiya 221, yako maang’amuzi haya. Mwaka 2011, Askofu Mkuu wa Madrid wakati huo, Kardinali Rouco Varela alituma jumuiya 10 za kwanza kwenye utume.

Askofu Mkuu wa sasa wa mji mkuu wa Hispania, Kardinali Carlos Osoro Sierra, katika mkutano wa Machi 22, 2015, alituma jumuiya 8 mpya. Huko Madrid, kuna jumla ya jumuiya 18 katika utume.

Tarehe 5 Mei 2018, Papa Fransisko, katika kuadhimisha miaka 50 ya kuzaliwa kwa jumuiya ya kwanza ya Njia huko Roma, katika mkutano mkubwa huko Tor Vergata (Roma) alituma jumuiya 25 kwenye utume kwa parokia mbalimbali za Roma ili kutegemeza na kuimarisha maisha ya kikristo ya jumuiya za parokia zenye magumu zaidi.

Leo, katika ‘nendeni’ hii ya Yesu, yamo mazingira na changamoto mpya za utume wa kuinjilisha wa Kanisa, na sote tumeitwa kwa “mtoko” huu mpya wa kimisionari. Kila mkristo na kila jumuiya itapambanua ipi ndiyo njia ambayo Bwana anaomba kwake, lakini sote tunaalikwa kukubali wito huu: kutoka katika raha yako na kuthubutu kuyafikia maeneo yote ya mbali yanayohitaji nuru ya Injili”.


Hatua za njia

Hatua za Njia ya Neokatekumenato

Uzuri mpya


Picha na madirisha

Madirisha ya vioo ya Kanisa Kuu la Almudena Madrid

Michoro katika Njia ya Neokatekumenato

Kiko Argüello alisomea Sanaa katika Chuo cha Mt. Fernando cha Madrid na mwaka 1959 alipokea Tuzo ya Kitaifa ya Pekee ya Uchoraji. Mnamo 1960, pamoja na mchongaji sanaa Coomontes na mchoraji wa vioo Muñoz de Pablos, alianzisha kikundi cha utafiti na maendeleo ya Sanaa Wakfu “Gremio 62”. Alifanya maonyesho huko Madrid (Maktaba ya Taifa), na kuiwakilisha Hispania, akiteuliwa na Wizara ya Utamaduni, katika Maonyesho ya Sanaa Takatifu Ulimwenguni huko Royan (Ufaransa) mwaka wa 1960. Huko Uholanzi, alionyesha baadhi ya kazi zake (Nyumba ya sanaa “Sura mpya”).


Taji la Kifumbo

Michoro Kanisa Kuu la Almudena Madrid

“Uzuri mpya peke yake utaokoa Kanisa». Picha za “taji la kifumbo” hili zinataka kupenya mpaka ndani kabisa ya roho ya mwumini azitazamazo. Zimekusudiwa kumsaidia mwanadamu kumuinukia Mungu. Picha hizi zinatenda juu rohoni mwa Mkristo kama kwenye Kugeuka Sura, ambapo mitume waliona mng’ao wa mwanga wa kimungu juu ya Mlima Tabori. Kama yeye, wanasikiliza Neno la Mungu, na zaidi ya yote katika liturjia, picha hizi, kwa njia ya moja kwa moja, hapo hapo na kwa hisia zaidi, zinataka kuwasaidia waumini kugeuka sura kiroho. Mtakatifu Yohane wa Dameski, ambaye alitetea michoro hii dhidi ya nguvu ya “iconoclasm” (mkondo uliokataza na kuharibu picha za kidini) na ambaye Papa Leo XIII alimtangaza kuwa Mwalimu wa Kanisa Zima, alisema: “Nimeona sura ya kibinadamu ya Mungu na nafsi yangu imeokolewa”

Sura Takatifu ya Kristo iwasaidie ninyi kuwa mashahidi wa upendo wake.

Kiko Argüello.


Usanifu Majengo

Usanifu Majengo katika Njia ya Neokatekumenato

Kanisa dogo la Sakramenti Takatifu Domus Galilaeae

Katika historia, Kanisa daima limekuwa na kifungo hiki kati ya uzuri na uinjilishaji, nalo Kanisa limekuwa mjumbe mkubwa zaidi wa uzuri. Kila kitu kinaakisi uzuri wa Kristo na uzuri wa jumuiya na wa ushirika wa kindugu. Uinjilishaji wa mataifa ya Waslavi (“Slavonic peoples”) ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa njia ya uzuri wa liturjia, wa picha na nyimbo. Ni katika miaka hii ya mwisho tu ambapo hata ndani ya Kanisa maono ya kitendaji yanaonekana kutawala ambayo yanapunguza mahali ambapo jumuiya inaishi na kukutana kuwa tu vyumba vya mikutano mkutano.

Walakini, hasa leo, zaidi kuliko hapo awali ni lazima na ya dharura kwamba miundo ya Kanisa ifanywe upya. Jibu kwa utandawazi (kijiji cha ulimwengu), kwa jiji kubwa, kwa “utamaduni mmoja”, ni parokia ambayo inakuwa “kijiji cha mbinguni”: mfano wa kijamii wa kibinadamu zaidi wenye uwezo wa kufungua nafasi kwa ajili ya jamii mpya ya upendo Kusanyiko la Ekaristi linalowawezesha waumini kushiriki kwa namna hai, uhalisia wa jumuiya ya jumuiya zenye “catecumenium” inayoundwa na kumbi za kupendeza za kiliturjia kwa maadhimisho katika jumuiya ndogo.

Katika mabara yote matano inawezekana kukutana na kazi zilizofanywa na Kiko ndani ya uzuri mpya: Seminari za Redemptoris Mater, parokia mpya, “catecumenium” (yaani, kumbi kwa maadhimisho ya jumuiya), nk.


Uchongaji sanaa

Uchongaji sanaa katika Njia ya Neokatekumenato

Hotuba ya Mlimani - Uchongaji

Dostoevsky, “Uzuri utaokoa ulimwengu.” Uzuri, kama mnavyojua, ni silka ya utu, pamoja na wema na ukweli. Kwa sababu, kama anavyosema Mtakatifu Thomaso, uhalisia wote ni mmoja, ni wa kweli, ni halisi. Lakini mimi ninapenda kuhusisha uzuri na raha. Hisia ya uzuri, urembo, hutupatia raha, hutufanya tusikie hisia. Kwa hiyo Mungu, kwa namna fulani, ameumba maumbile. Aliyeumba maumbile, ameyafanya kuwa mazuri ili kutupatia raha.

Raha inahusiana na upendo. na inavutia, kwangu mimi kama mchoraji, niliyesomea sheria za uwiano, kwamba kila kitu katika maumbile kinahusiana na uzuri, na kipo kwa ajili ya uzuri. Si kila kitu ni uzuri, kwa maana fulani, lakini sheria za uwiano zinahusiana katika maada, katika umbo… Inaamsha shauku, sayansi inayosoma mahusiano ni hisabati, ndiyo maana katika uwiano kuna mfuatano mzima wa milinganyo ambayo ni ya kihisabati. Tayari katika sanaa ya Plato alizungumza juu ya jiometria ya uumbaji na ya hisabati. Katika sanaa, iwe katika uchoraji, iwe katika uchongaji, iwe katika muziki, iwe katika ushairi, kila kitu kiko kwenye uhusiano, mahusiano ambayo yanapatana.

Tabenakulo ya Domus Galilaeae

Uhusiano huu wa kihisabati uliopo katika uwiano, upo vilevile katika wakati, upo katika muziki. Muziki ni muhimu sana kwa sababu unatufundisha uzuri katika mgawanyiko wa muda. Kila nota inatoa thamani ya nota inayofuata katika wakati, katika uchoraji kila kitu, kila mumbile , kila nyenzo, kila mchoro unathamini mwingine. Kwa mfano, simfonia ya nne ya Beethoven, inaanza na “dissonance” (nota zisizoendana). Ni ajabu. Kuthamini muda ndani ya wakati, tuseme kwamba kuna … Tusiseme juu ya ushairi, neno, uchongaji. Kwa mfano, Henry Moore, mchongaji sanaa mwingereza, amesomea mifupa ya mwanadamu, na ameona kwamba mifupa ya mtu … Pengo ndani ya mfupa wa paja ni kamilifu. Pengo hilo ni kamilifu kwa ajili ya kazi ya uungaji wa mifupa na wakati huo huo unapendeza, hadi kiwango cha juu. Kutengeneza tao lenye uzuri, linalopendeza, ni vigumu sana. Tao la shingo ya sili ni ya ajabu. Jinsi wanyama wanavyohusiana, sio kila tao lina uzuri. Moore anachukua mapengo haya, anayasoma na kutengeneza sanamu yenye matao, kwa sababu tao la aina fulani linaendana na uvimbe mwingine wa aina nyingine ili kuleta uzuri, kwa sababu kila kitu kinahusiana.

Tuseme hivi kwamba katika uzuri kuna siri ya kina, ambayo ni upendo.

Kiko ametengeneza vifaa vingi kwa ajili ya liturjia: vikombe, sahani, vyetezo, vifuniko vya Biblia, mapambo…, na pia sanamu nyingi: Hotuba ya Mlimani, Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili, Yesu Kristo msulubiwa, paa nk.


Vitabu

Wasifu wa Maisha – Carmen Hernández

 Kununua
Carmen Hernández. Wasifu ya maisha na Aquilino Cayuela.

Katika maelezo haya ya wasifu mtamwona mwanamke wa kipekee, muhimu sana kwa Kanisa, aliyeshikwa upendo na Kristo, na Maandiko na pia na Ekaristi. Alijua wazi kwamba utume ambao Mungu alikuwa amempa ulikuwa kuniunga mkono, kunitetea na kunisahihisha, kwa manufaa ya Njia ya Neokatekumenato. Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya Carmen ambaye daima ameniambia ukweli. Alikuwa mwanamke wa kina, halisi na huru katika uhusiano wake na kila mtu. Alikuwa na akili sana. Alimpenda Kristo na Kanisa na Papa, zaidi ya yote. Tunaamini kwamba Carmen yuko pamoja na Bwana, tayari yuko kwenye sherehe. Maelezo haya ya wasifu si tu kwa ajili ya ndugu wa Njia, bali ni kwa ajili ya Kanisa zima, kumtambulisha mwanamke wa ajabu, ambaye ameishi imani kwa kiwango cha kishujaa. Carmen Hernandez! (Kiko Arguello).

Wasifu rasmi wa kwanza wa Carmen Hernández umechapishwa. Kumbukumbu ya miaka mitano ya kufariki kwake Carmen Hernández, Julai 19, 2021, inalingana na kuchapishwa kwa wasifu wake rasmi wa kwanza, ambaye mwandishi wake ni profesa na daktari wa Falsafa Aquilino Cayuela na umehaririwa na Maktaba ya Waandishi wa Kikristo (BAC).


Kerigma. Katika vibanda pamoja na maskini.

 Kununua

“Nimetaka kuandika kitabu hiki kidogo kilichopendekezwa na Kardinali Cañizares, ambaye aliona ni muhimu niseme kitu kuhusu yale ambayo Bwana amefanya nasi katika vibanda, pamoja na maskini, na pia kwamba ningechapisha kerigma ambayo itaweza kusaidia, hasa kwa upande wa maudhui na wa anthropolojia, kwa ajili ya Sinodi juu ya Uinjilishaji Mpya». Kiko Arguello.

Kardinali Cañizares: «Kitabu hiki ni zawadi kweli ya Mungu, kinachotuhuisha na kututia moyo katika imani, kinachoondoa hofu na kutujaza ujasiri.

Kardinali Schönborn: “Katika katekesi hii, kwa namna ya ajabu, tangazo zima la Injili limefupishwa”.


Noti 1988-2014

 Kununua

“Tangu karibu miaka thelathini iliyopita, nimekuwa nikiandika kwenye daftari, mara kwa mara na bila utaratibu, na bila nia iliyodhamiriwa, baadhi ya mawazo, tafakari, kweli, kumbukumbu, fikira, maelezo, mazungumuzo ya nafsi, maombi, n.k., yaliyoamshwa ndani yangu wakati wa utume wa uinjilishaji na wa katekesi ambayo kwayo Bwana ameniita katika Kanisa, pamoja na Carmen Hernández na Pd. Mario Pezzi. Ikiwa noti hizi zinamsaidia mtu, Mungu na ahimidiwe”.

“Kitabu hiki kimeundwa na vipande vidogo vya fasihi ambavyo vinaweza kusomwa bila kuunganishwa na kile kilichotangulia au kinachofuata. Ni tafakari zilizotokana na tukio, kuishi pamoja au mkutano; kubisha mlango wa roho kwa kutangaza au kujishtaki; kujiuliza au kujiita kwa matumaini ambako msomaji anajisikia kuhusishwa: mara nyingi ni siri za kuthubutu zinazotoka katika nafsi ya mwandishi; wakati mwingine ni aina ya tenzi au zaburi, dua zenye moto na shukrani za kusisimua kwa Mungu. Kwa maelezo yaliyomo kwenye maandishi mafupi haya inawezekana kwa namna fulani kufuata mkondo wa kihistoria kutoka 1988 hadi 2014. Yanaunganishwa na historia ya imani ya mwandishi na ya Njia ya Neokatekumenato, zaidi kuliko uendelezaji wa mada, ingawa maudhui mengi ya karama husika yanaonekana hapa na pale. Ni historia iliyojaa furaha na mateso; inaruhusu kuona pambano la mwandishi kwa kutekeleza kwa uaminifu agizo lililopokelewa kutoka kwa Mungu» († Mons. Ricardo Blázquez Pérez, Kardinali Askofu Mkuu wa Valladolid).


Shajara za 1979-1981

 Kununua
Shajara za 1979-1981

“Kunanyesha, lakini siku inapambazuka tulivu. Yesu, nashangaa. Asante. Mateso yameweka huruma moyoni mwangu. Asante Yesu. Amani, furaha…”. Carmen Hernández, Bonde la Walioanguka – Madrid, Januari 27 kutoka 1979.

“Miaka hamsini bila kusimama hata mara moja, safari, uchunguzi, kutembelea jumuiya nyingi huko Madrid, Zamora, Barcelona, Paris, Roma, Florence, Ivrea… Kusikiliza na kusikiliza kila ndugu kuhusu maisha yake, mateso yake na historia yake, ikiangazwa kwa nuru ya imani, ya msalaba mtukufu wa Bwana Wetu Yesu. Nafikiri kwamba mna haki ya kuufahamu moyo wake Carmen, upendo wake mkuu kwa Yesu Kristo. Alisema mara daima: “Yesu wangu, nakupenda, nakupenda. Njoo, njoo, nisaidie»» (Kiko Argüello).


Njia ya Neokatekumenato

Njia ya Neokatekumenato - Maneno ya Mapapa

Maneno ya Mapapa: Paulo VI, S. Yohane Paulo II, Benedikto XVI na Fransisko.

Mitume wa kwanza, katika vikundi vidogo vya uinjilishaji, walizunguka katika masinagogi wakitangaza Habari Njema: Mungu amemfufua mtumishi wake Yesu, ambaye sisi tumemkana, tukiomba neema kwa mwuaji; yule aliyekufa bila kuweka pingamizi, bila kushindana na uovu, akiwapenda adui zake, asiwahesabie makosa (“Wasamehe kwa sababu hawajui watendalo”); yule aliyetoa sadaka mabaya waliyomfanyia -mateso na msalaba – kama uthibitisho wa kwamba upendo wake ulikuwa mkubwa kuliko mauti na kwamba hakuacha kuwapenda, hata kama wangechukua uhai wake: Mungu alimfufua kutoka mauti na leo Yeye yu hai, ili kusamehe kosa hili na lingine lolote.

“Muda wetu unahitaji kuanza upya ujenzi wa Kanisa, karibu kisaikolojia na kichungaji, kana kwamba lingeanza tena, kutoka mwanzo, kwa kusema hivi, kuzaliwa upya» Paul VI, Hotuba ya Jumatano, Agosti 4, 1976.


Nyimbo za Njia ya Neokatekumenato

Kitabu cha Nyimbo Amefufuka

Imepitiwa na Senta ya Neokatekumenato ya Jimbo la Madrid. Kitabu cha nyimbo kimehaririwa kwa rangi mbalimbali ili kutofautisha hatua za mihula ya Njia. Waimbaji wanapswa kuchagua nyimbo kulingana na hatua ya Njia ambamo Jumuiya yao imo na kusubiri makatekista wawapitishie nyimbo katika Kuishi Pamoja mbalimbali na Hatua za Njia, kwa njia hii ndugu wanaweza kuelewa maana ya kila wimbo.


Orkestra

Orkestra ya Kisimfonia ya Njia ya Neokatekumenato imeanzishwa kama huduma ya Njia ya Neokatekumenato kwa uinjilishaji kupitia muziki.

Orkestra ya Kisinfonia ya Njia ya Neokatekumenato