Mmewasha moto wa Injili pale ambapo ulionekana kuzimika.
Papa Leo XIV

Papa Leo XIV akutana na Makatekista 1.000 kutoka Njia ya Neokatekumenato
Asubuhi ya leo, 19 Januari 2026, Baba Mtakatifu Leo XIV, katika “Ukumbi wa Baraka” aliwapokea makatekista wasafiri zaidi ya 1,000, wawajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato katika mataifa 138 katika mabara yote matano.
Mwishoni mwa kuishi pamoja, iliyofanyika katika Kituo cha “Mtumishi wa Yahweh” huko Porto San Giorgio (Italia), chini ya mwongozo wa kikundi cha wawajibikaji wa Njia duniani kote, Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi na María Ascensión Romero, wamekutana mjini Roma kwa mkutano wao wa kwanza pamoja na Baba Mtakatifu Leo XIV.
Katika kuishi pamoja, kama inavyofanyika kila mwaka tangu mwanzo wa Njia , wameshirikishana maang’amuzi ya uinjilishaji ambao Njia inatekeleza katika zaidi ya parokia 6,200 katika majimbo 1,408 ulimwenguni, ili kuhimiza uingizwaji wa kikristo, chombo kinachowasaidia maaskofu na mapadre wa nchi mbalimbali katika kazi ya tangazo la Injili katika dunia ya leo.
Pia walihudhuria mkutano huo na pamoja na Baba Mtakatifu magombera 115 wa Seminari za Kijimbo za Kimisionari ambazo Njia imesaidia kufungua katika majimbo mengine mengi zaidi, pamoja na walezi wapatao mia.
Katika kuishi pamoja imewezekana kuthibitisha, kupitia maang’amuzi mbalimbali katika mabara tofauti, hali ngumu ambamo Kanisa la leo limeitwa kuendeleza utume wake. Katika muktadha huu wa kidunia, imeonekana waziwazi kwamba Njia ya Neokatekumenato imeitwa kuchangia katika amani na maelewano kati ya watu, ikileya matumaini ya tangazo la kikristo, la kerygma, na ikiunda jumuiya za kikristo zenye uwezo wa kutoa ishara za imani kwa kizazi hiki, upendo na umoja.
Kufika na kuondoka kwa Papa kumesindikizwa na makofi mengi na shangwe, kama vile nyimbo za Kiko Argüello ambazo kusanyiko zima limeimba kwa shauku.
Kiko amempa Baba Mtakatifu nakala ya mchoro wa Mchungaji Mwema, uliochorwa na yeye mwenyewe mwaka 1982. Aidha, na kwa wakati mwafaka, kwa vile Papa amepanga ziara huko Hispania katika miezi ijayo, Kiko amempa pia makala kuhusu Kanisa Kuu la Madrid, Bikira Maria Mama wa Almudena, ambapo mwaka 2004 Kiko alichora “taji la kifumbo” (mpangilio wa michoro mbalimbali inayoeleza historia ya wokovu katika Kristo), pamoja na madirisha ya vioo yenye michoro yaliyoko kwenye dari juu ya madhabahu.
Papa Leo alisema nao waliohudhuria kwa maneno yafuatayo:
Ningependa kutoa shukrani zangu kwa familia zote ambazo, kwa kukaribisha msukumo wa ndani wa Roho, wanaacha usalama wa maisha ya kawaida na kuondoka katika utume, hata katika maeneo ya mbali na magumu, kwa hamu tu ya kutangaza Injili na kuwa mashahidi wa upendo wa Mungu.
Vikundi vya wamisionari wasafiri, vilivyounda na familia, makatekista na mapadre, wanashiriki katika utume wa Kanisa zima wa kuinjilisha na… vinachangia “kuamsha” imani ya wasio wakristo ambao hawajawahi kusikia habari za Yesu Kristo.
Kuishi maang’amuzi ya Njia ya Neokatekumenato na kutekeleza utume huo kunadai pia, kwa upande wenu, kuwa macho ndani yenu na uwezo wa kupambanua kwa hekima, ili kutambua baadhi ya hatari ambazo daima zinatishia maisha ya kiroho na ya kikanisa .
Karama zinawekwa daima kwa huduma ya Ufalme wa Mungu na ya Kanisa pekee la Kristo, ambamo hakuna kipawa cha Mungu kilicho muhimu zaidi kuliko vingine.
Mema mnayofanya ni makubwa, kwa sababu kusudi lake ni kuwawezesha watu kumjua Kristo.
Songeni mbele kwa furaha na unyenyekevu, bila kujitenga, kama wajenzi na mashahidi wa ushirika.
Wapendwa, nawashukuru kwa juhudi yenu, kwa ushuhuda wenu wenye furaha na kwa huduma mnayotoa katika Kanisa na duniani. Ninawatia moyo mwendelee kwa shauku na ninawabariki, huku nikiita juu yenu maombezi ya Bikira Maria ili awasindikize na kuwalinda. Asanteni!
