Maadhimisho ya Miaka 60 ya Njia ya Neokatekumenato na Tukio la Kufungwa kwa Awamu ya Kijimbo ya Mchakato wa Kumtangaza Carmen Hernández kuwa Mtakatifu

Madrid. Kardinali Cobo Cano ataongoza Misa Takatifu katika maadhimisho ya miaka 60 ya Njia ya Neokatekumenato na Tukio la kufunga awamu ya kijimbo ya mchakato wa kumtangaza Mtumishi wa Mungu Carmen Hernández kuwa mwenye heri. Siku ya Jumamosi, Mei 30, saa 2:00 usiku, Kardinali José Cobo Cano, Askofu Mkuu wa Madrid, ataongoza adhimisho la Ekaristi katika Kathedrali ya Bikira Maria Mama Yetu wa Almudena, ili kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 60

Ufunguzi wa Mchakato wa Kutangazwa Mwenye Heri kwa Mtumishi wa Mungu Carmen Hernández

“Yesu wangu, nipeleke kwenye utakatifu wako”; “Wewe unaniongoza kwenye utakatifu” (“Kitabu cha kumbukumbu 1979-1981”, na. 85; na.199) Tarehe Desemba 4, 2022, “Tukio” lenye nguvu na maana maalum kwa Kanisa zima lilitukia huko Madrid: ufunguzi wa hatua ya kijimbo ya Kutangazwa Mwenye Heri na Kutangazwa Mtakatifu kwa Carmen Hernández Barrera, mwanzilishi mwenza, pamoja na Kiko Argüello, wa njia hiyo ya uanzishwaji wa kikristo inayoitwa Njia ya Neokatekumenato. Ufunguzi wa mchakato Katika

Papa Fransisko ampongeza Kiko Argüello kwa kutimiza miaka 81 ya uhai

Papa Fransisko alimpigia simu mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato, Kiko Argüello, alasiri ya tarehe 9 mwezi Januari ili kumpongeza kwa kutimiza miaka 81 ya uhai. Fransisko alitumia fursa hiyo kwa ajili ya kumsalimia na kumwahidia kwa mara nyingine tena kwamba atamtegemeza yeye pamoja na Njia nzima ya Neokatekumenato, akimhimiza kuendelea kusonga mbele. Kiko, akishangazwa na zawadi hiyo kutoka kwa Baba Mtakatifu, alimshukuru sana kwa tendo hilo na alifanya upya utii