Ufunguzi wa Mchakato wa Kutangazwa Mwenye Heri kwa Mtumishi wa Mungu Carmen Hernández

“Yesu wangu, nipeleke kwenye utakatifu wako”; “Wewe unaniongoza kwenye utakatifu” (“Kitabu cha kumbukumbu 1979-1981”, na. 85; na.199) Tarehe Desemba 4, 2022, “Tukio” lenye nguvu na maana maalum kwa Kanisa zima lilitukia huko Madrid: ufunguzi wa hatua ya kijimbo ya Kutangazwa Mwenye Heri na Kutangazwa Mtakatifu kwa Carmen Hernández Barrera, mwanzilishi mwenza, pamoja na Kiko Argüello, wa njia hiyo ya uanzishwaji wa kikristo inayoitwa Njia ya Neokatekumenato. Ufunguzi wa mchakato Katika

Papa Fransisko ampongeza Kiko Argüello kwa kutimiza miaka 81 ya uhai

Papa Fransisko alimpigia simu mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato, Kiko Argüello, alasiri ya tarehe 9 mwezi Januari ili kumpongeza kwa kutimiza miaka 81 ya uhai. Fransisko alitumia fursa hiyo kwa ajili ya kumsalimia na kumwahidia kwa mara nyingine tena kwamba atamtegemeza yeye pamoja na Njia nzima ya Neokatekumenato, akimhimiza kuendelea kusonga mbele. Kiko, akishangazwa na zawadi hiyo kutoka kwa Baba Mtakatifu, alimshukuru sana kwa tendo hilo na alifanya upya utii