Papa anampokea Kiko Argüello, mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato

Asubuhi ya leo, Jumamosi, tarehe 27 Januari 2024, Papa Fransisko aliwapokea katika hadhira binafsi Kikundi cha Kimataifa cha wajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato: mwanzilishi Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi na Ascensión Romero. Katika hadhira hiyo, Kikundi walimjulisha Baba Mtakatifu kuhusu Kuishi Pamoja ya Kiulimwengu, ambayo imehitimishwa hivi punde, ikiwa na zaidi ya makatekista wasafiri 1,000, wanaowajibika kwa mataifa 136 ambapo Njia ya Neokatekumenato ipo, na Magombera wa Seminari za Kimisionari

Maoni mubashara katika hafla ya ufunguzi wa mchakato ya Kutangazwa kuwa Mwenye Heri kwa Carmen Hernández

Maoni ya Kiko Argüello Jioni njema kwenu nyote, Namsalimu Mha. Carlos Osoro, Kardinali-Askofu Mkuu wa Madrid. Mwadhama Kardinali Antonio Maria Rouco, Askofu Mkuu Mstaafu wa Madrid. Kardinali Paolo Romeo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Palermo. Maaskofu wakuu, maaskofu na maaskofu wasaidizi waliopo hapa. Mama Mkuu wa Wamisionari wa Kristo Yesu na washauri wake. Ni furaha gani unayotupatia uwepo wenu katika hafla hii, madada! Mkuu wa Chuo, Pd. Daniel Sada, Wakuu wa

Ufunguzi wa Mchakato wa Kutangazwa Mwenye Heri kwa Mtumishi wa Mungu Carmen Hernández

“Yesu wangu, nipeleke kwenye utakatifu wako”; “Wewe unaniongoza kwenye utakatifu” (“Kitabu cha kumbukumbu 1979-1981”, na. 85; na.199) Tarehe Desemba 4, 2022, “Tukio” lenye nguvu na maana maalum kwa Kanisa zima lilitukia huko Madrid: ufunguzi wa hatua ya kijimbo ya Kutangazwa Mwenye Heri na Kutangazwa Mtakatifu kwa Carmen Hernández Barrera, mwanzilishi mwenza, pamoja na Kiko Argüello, wa njia hiyo ya uanzishwaji wa kikristo inayoitwa Njia ya Neokatekumenato. Ufunguzi wa mchakato Katika

Ufunguzi wa Mchakato wa Kutangazwa Mwenye Heri na Kutangazwa Mtakatifu wa Carmen Hernández

Mubashara Kutoka Madrid (Hispania), jumapili tarehe 4 Desemba, 2022,  saa 2 usiku, East Africa Time (GMT +03:00)  Jimbo Kuu la Madrid Kituo cha michezo cha Chuo Kikuu cha Francisco Vitoria. Anaongoza ibada Kard. Carlos Osoro, Askofu Mkuu wa Madrid. Waanzilishi wa Mchakato: Kiko Argüello, P. Mario Pezzi, Ascensión Romero, Taasisi za “Familia ya Nazareti” za Roma na Madrid. Mwombaji: Carlos Metola.

Kusali kwa kupitia maombezi ya Carmen Hernández

Alizaliwa Ólvega (Soria) tarehe 24 Novemba 1930 na aliishi utotoni mwake huko Tudela (Navarra). Tangu alipokuwa mtoto, alisikia wito wa kimisionari , akivutiwa na roho ya Mt. Fransisko Ksaveri. Alisomea Sayansi za Kemia katika Chuo Kikuu cha Madrid. Kwa miaka kadhaa alikuwa sehemu ya “Taasisi ya Kimisionari ya Kristo Yesu” na alisoma Teolojia huko Valencia. Mwaka 1964 alimfahamu Kiko Argüello katika vibanda vya Palomeras Altas huko Madrid, na baada ya