Nuru ya Bikira Maria Mkingiwa yang’aa huko Oviedo
Njia ya Neokatekumenato inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 50 huko Oviedo (Hispania) kwa uwepo wa Kiko Argüello na Askofu Mkuu Mha. Jesús Sanz Montes. Tamasha huko Oviedo Ili kuadhimisha miaka 50 ya Njia ya Neokatekumenato huko mkoani Asturias, katika mji wa Oviedo, Askofu Mkuu Mons. Jesús Sanz Montes aliongoza Mkesha wa Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili pamoja na jumuiya za Neokatekumenato za mji huo mkuu Mkoa wa Asturias.