Njia ya Neokatekumenato: “Mchango wenye thamani kwa maisha ya Kanisa”

Mmewasha moto wa Injili pale ambapo ulionekana kuzimika.  Papa Leo XIV Papa Leo XIV akutana na Makatekista 1.000 kutoka Njia ya Neokatekumenato Asubuhi ya leo, 19 Januari 2026, Baba Mtakatifu Leo XIV, katika “Ukumbi wa Baraka” aliwapokea makatekista wasafiri zaidi ya 1,000, wawajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato katika mataifa 138 katika mabara yote matano. Mwishoni mwa kuishi pamoja, iliyofanyika katika Kituo cha “Mtumishi wa Yahweh” huko Porto San Giorgio (Italia),

Papa Leo XIV ampokea Kiko Argüello, mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato

Leo asubuhi, tarehe 5 Juni 2025, saa tano asubuhi, katika Maktaba ya Ikulu ya Kitume, Baba Mtakatifu Leo XIV amepokea kwa mara ya kwanza kwa faragha Kikundi cha Kimataifa ya Njia ya Njia ya Neokatekumenato, Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi, na María Ascensión Romero. Kiko alimsalimia Papa, akimwambia kwamba alikuwa na furaha sana kwamba Mungu ametupa Papa mmisionari, kwa sababu hii pia ndio utume wa Njia ya Neokatekumenato, katika nchi

Uchaguzi wa Papa Leo XIV

Njia ya Neokatekumenato imepokea habari za kuchaguliwa kwa Kardinali Robert Prevost kuwa Khalifa wa Petro kwa furaha kubwa. Maneno yake ya kwanza yametujaza furaha, akimweka Kristo Mfufuka kama kiini cha yote, ambaye anatupatia amani yake, pamoja na uinjilishaji unaozaliwa kutoka katika moyo wa kimisionari. Kumekuwa na mwangwi wa pekee katika mioyo ya ndugu wote wa Njia—na hasa ule wa kwangu— kutokana na kwamba uchaguzi huu ulifanyika siku ya Bikira Maria