Onyesho la kimuziki kwa ajili ya Jubilei ya Familia

Kazi ya Kisinfonia ya Kiko Argüello pamoja na Orkestra ya Njia ya Neokatekumenato, ikiwa imeongozwa na Tomáš Hanus Jubilei 2025 Jumapili, Juni 1, 2025, saa moja jioni, katika Ukumbi wa “Parco della Música Ennio Morricone”, kwenye Ukumbi wa Santa Cecilia, Kiko Argüello awasilisha Kazi yake ya Kisinfonia. Onyesho juu kwa ajili ya Jubilei ya Familia, ambapo Orkestra ya Njia ya Neokatekumenato, inayoendeshwa na Tomáš Hanus, mkurugenzi wa Orkestra ya Kisinfonia

Uchaguzi wa Papa Leo XIV

Njia ya Neokatekumenato imepokea habari za kuchaguliwa kwa Kardinali Robert Prevost kuwa Khalifa wa Petro kwa furaha kubwa. Maneno yake ya kwanza yametujaza furaha, akimweka Kristo Mfufuka kama kiini cha yote, ambaye anatupatia amani yake, pamoja na uinjilishaji unaozaliwa kutoka katika moyo wa kimisionari. Kumekuwa na mwangwi wa pekee katika mioyo ya ndugu wote wa Njia—na hasa ule wa kwangu— kutokana na kwamba uchaguzi huu ulifanyika siku ya Bikira Maria

Maaskofu katika Nchi Takatifu wakialikwa na Njia ya Neokatekumenato

Maaskofu na maaskofu wakuu mia mbili na hamsini kutoka mabara matano, wakisindikizwa na wamisionari wasafiri, mapadre na walei, pamoja na kikundi cha wajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato katika majimbo yao (jumla ya ndugu zaidi ya 500), walialikwa na kikundi cha kimataifa cha wajibikaji wa Njia -Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi na Ascensión Romero- katika mkutano huko Nchi Takatifu. Mwaliko huo kwa Nchi Takatifu ulithibitishwa na barua kutoka kwa Mwadhama Kardinali

Tangazo kutoka kwa Njia ya Neokatekumenato kutokana na kufariki kwake Papa Fransisko

21 Aprili 2025 Kiko, Padre Mario na Ascensión, wajibikaji duniani wa Njia ya Neokatekumenato, pamoja na Ndugu wote wa Njia wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu, Papa wetu Fransisko. Jana, katika ujumbe wake wa Pasaka Urbi et Orbi (maana yake “kwa mji (Roma) na kwa dunia nzima”), ametupatia ushuhuda wake wa mwisho wa imani: “Ndugu wapendwa: Katika Pasaka ya Bwana, kifo na uzima zimekabiliana katika pambano la ajabu,

App ya kitabu cha nyimbo «AMEFUFUKA» inapatikana sasa.

Tunayo furaha ya kutangaza kwamba aplikesheni rasmi ya Kitabu cha Nyimbo “AMEFUFUKA” sasa inapatikana kwa usakinishaji, katika lugha kadhaa, kwenye vifaa vya Android na iOS (Apple): Aplikesheni hii mpya inatoa namna rahisi na inayoweza kufikiwa ili kutafuta na kupata nyimbo zote kutoka kwa “AMEFUFUKA”, iliyo bora kwa waimbaji wa jumuiya na ndugu wengine ambao wangependa kuwa na nyimbo kamili karibu. Ni hapa pekee, ambapo mtaweza kupata matoleo rasmi ya nyimbo zote,

Moyo usiogawanyika, utume na ubikira katika Carmen Hernández

Kimechapishwa kitabu kipya kuhusu Carmen, mwanzilishi mwenza pamoja na Kiko  Argüello wa Njia ya Neokatekumenato, na kinastahili kuzingatiwa nasi. Tunsaema kuhusu kitabu kinachoitwa Corazón Indiviso, misión y virginidad en Carmen Hernández, (“Moyo Usiogawanyika, utume na ubikira katika Carmen Hernández”) iliyoandikwa na Josefina Ramón, mshiriki katika Njia wa Neokatekumenato, na ambaye, kwa kufuata nyayo za Carmen, ni pia mseja na mmisionari msafiri, na kwa kuwa alilishwa na maisha na utajiri wa