Njia ya Neokatekumenato na Jubilei

Ushuhuda wa Kiko Argüello. Pentekoste 2025 Naitwa Kiko Argüello na, pamoja na Mtumishi wa Mungu, Carmen Hernández, sisi ni waanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato, utaratibu wa kijimbo wa uingizwaji wa kikristo ambao – kupitia katekesi, Neno la Mungu na sakramenti zinazoshirikiwa katika jumuiya – huwaongoza watu kuishi imani kipevu na ushirika wa kindugu. Mimi ni mchoraji mhispania. Wakati wa miaka yangu ya chuo kikuu, baada ya dhahama kubwa ya kiutu,

Papa Leo XIV ampokea Kiko Argüello, mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato

Leo asubuhi, tarehe 5 Juni 2025, saa tano asubuhi, katika Maktaba ya Ikulu ya Kitume, Baba Mtakatifu Leo XIV amepokea kwa mara ya kwanza kwa faragha Kikundi cha Kimataifa ya Njia ya Njia ya Neokatekumenato, Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi, na María Ascensión Romero. Kiko alimsalimia Papa, akimwambia kwamba alikuwa na furaha sana kwamba Mungu ametupa Papa mmisionari, kwa sababu hii pia ndio utume wa Njia ya Neokatekumenato, katika nchi

Kazi za Kisimfonia ya Kiko Argüello: Njia ya Uzuri kwa ajili ya Uinjilishaji

Tafsiri yetu ya makala iliyochapishwa kwa idhini ya Vatican News Kutokana na hafla ya Jubilei ya Familia, simfonía zote mbili za mwanzilishi wa Njia ya Neokatekumenato, zilipigwa pamoja kwa mara ya kwanza jioni ya Juni 1, 2025, kwenye “Auditorio Parco della Musica” (“Ukumbi wa Bustani ya Muziki”)huko Roma: Monsinyori Fisichella asema: simfonia ya aina hii imetufundisha kuwa sisi si watazamaji bali washiriki. Débora Donnini – Mji wa Vatikano  Ni muziki

Onyesho la kimuziki kwa ajili ya Jubilei ya Familia

Kazi ya Kisimfonia ya Kiko Argüello pamoja na Orkestra ya Njia ya Neokatekumenato, ikiwa imeongozwa na Tomáš Hanus Jubilei 2025 Jumapili, Juni 1, 2025, saa moja jioni, katika Ukumbi wa “Parco della Música Ennio Morricone”, kwenye Ukumbi wa Santa Cecilia, Kiko Argüello awasilisha Kazi yake ya Kisimfonia. Onyesho juu kwa ajili ya Jubilei ya Familia, ambapo Orkestra ya Njia ya Neokatekumenato, inayoendeshwa na Tomáš Hanus, mkurugenzi wa Orkestra ya Kisimfonia

Uchaguzi wa Papa Leo XIV

Njia ya Neokatekumenato imepokea habari za kuchaguliwa kwa Kardinali Robert Prevost kuwa Khalifa wa Petro kwa furaha kubwa. Maneno yake ya kwanza yametujaza furaha, akimweka Kristo Mfufuka kama kiini cha yote, ambaye anatupatia amani yake, pamoja na uinjilishaji unaozaliwa kutoka katika moyo wa kimisionari. Kumekuwa na mwangwi wa pekee katika mioyo ya ndugu wote wa Njia—na hasa ule wa kwangu— kutokana na kwamba uchaguzi huu ulifanyika siku ya Bikira Maria

Maaskofu katika Nchi Takatifu wakialikwa na Njia ya Neokatekumenato

Maaskofu na maaskofu wakuu mia mbili na hamsini kutoka mabara matano, wakisindikizwa na wamisionari wasafiri, mapadre na walei, pamoja na kikundi cha wajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato katika majimbo yao (jumla ya ndugu zaidi ya 500), walialikwa na kikundi cha kimataifa cha wajibikaji wa Njia -Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi na Ascensión Romero- katika mkutano huko Nchi Takatifu. Mwaliko huo kwa Nchi Takatifu ulithibitishwa na barua kutoka kwa Mwadhama Kardinali

Tangazo kutoka kwa Njia ya Neokatekumenato kutokana na kufariki kwake Papa Fransisko

21 Aprili 2025 Kiko, Padre Mario na Ascensión, wajibikaji duniani wa Njia ya Neokatekumenato, pamoja na Ndugu wote wa Njia wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu, Papa wetu Fransisko. Jana, katika ujumbe wake wa Pasaka Urbi et Orbi (maana yake “kwa mji (Roma) na kwa dunia nzima”), ametupatia ushuhuda wake wa mwisho wa imani: “Ndugu wapendwa: Katika Pasaka ya Bwana, kifo na uzima zimekabiliana katika pambano la ajabu,