Shahada ya Udaktari wa Hesima “Honoris causa” yatolewa kwa Pd. Mario Pezzi

Siku ya Alhamisi, Novemba 13, Padre Mario Pezzi, mpresbiteri wa Kikundi cha Kimataifa cha Njia ya Neokatekumenato, atapokea Shahada ya Udaktari wa Heshima ya Theolojia kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Mt. Antonio cha Murcia (UCAM). Heshima hiyo itatotelwa ndani ya hafla ya ufunguzi wa mwaka wa masomo wa 2025-2026, mbele ya Monsinyori José Manuel Lorca Planes, Askofu wa Jimbo la Cartagena-Murcia, María Dolores García Mascarell, Rais wa UCAM, Josefina

“Tuzo Maalum ya Mwaka” katika gazeti la kidijitali “Religión en Libertad” yatolewa kwa Kiko Argüello

Jumatano tarege 29 Oktoba 2025 (Madrid, Hispania) RATIBA 19:30: Mwanzo wa hafla. Utambulisho kutoka kwa Álex Navajas na Sandra Segimon. Kukabidhi tuzo: 20:45: Mwisho wa hafla na wageni waalikwa kuagwa.

Ufafanuzi wa Njia ya Neokatekumenato + Nyongeza

Njia ya Neokatekumenato ni safari ya malezi ya kikatoliki inayotekelezwa katika majimbo kupitia huduma za bure (taz. Kifungu cha 4 cha Statuta za Njia ya Neokatekumenato), iliyoidhinishwa na Kiti Kitakatifu. Mikusanyiko ya maadhimisho ya jumuiya hutumia nyenzo mbalimbali (nyimbo, ishara za kiliturujia na michoro), ambazo ni matunda ya ubunifu wa Kiko Argüello na Carmen Hernández, ambao, bila kutafuta faida, wamezifanya zipatikane bila gharama yoyote kwa ndugu wa jumuiya na parokia

Uchaguzi wa Papa Leo XIV

Njia ya Neokatekumenato imepokea habari za kuchaguliwa kwa Kardinali Robert Prevost kuwa Khalifa wa Petro kwa furaha kubwa. Maneno yake ya kwanza yametujaza furaha, akimweka Kristo Mfufuka kama kiini cha yote, ambaye anatupatia amani yake, pamoja na uinjilishaji unaozaliwa kutoka katika moyo wa kimisionari. Kumekuwa na mwangwi wa pekee katika mioyo ya ndugu wote wa Njia—na hasa ule wa kwangu— kutokana na kwamba uchaguzi huu ulifanyika siku ya Bikira Maria

Maaskofu katika Nchi Takatifu wakialikwa na Njia ya Neokatekumenato

Maaskofu na maaskofu wakuu mia mbili na hamsini kutoka mabara matano, wakisindikizwa na wamisionari wasafiri, mapadre na walei, pamoja na kikundi cha wajibikaji wa Njia ya Neokatekumenato katika majimbo yao (jumla ya ndugu zaidi ya 500), walialikwa na kikundi cha kimataifa cha wajibikaji wa Njia -Kiko Argüello, Padre Mario Pezzi na Ascensión Romero- katika mkutano huko Nchi Takatifu. Mwaliko huo kwa Nchi Takatifu ulithibitishwa na barua kutoka kwa Mwadhama Kardinali

Tangazo kutoka kwa Njia ya Neokatekumenato kutokana na kufariki kwake Papa Fransisko

21 Aprili 2025 Kiko, Padre Mario na Ascensión, wajibikaji duniani wa Njia ya Neokatekumenato, pamoja na Ndugu wote wa Njia wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu, Papa wetu Fransisko. Jana, katika ujumbe wake wa Pasaka Urbi et Orbi (maana yake “kwa mji (Roma) na kwa dunia nzima”), ametupatia ushuhuda wake wa mwisho wa imani: “Ndugu wapendwa: Katika Pasaka ya Bwana, kifo na uzima zimekabiliana katika pambano la ajabu,